Onyo la Tsunami lafutwa New Zealand na New Caledonia
New Zealand imeshusha kiwango chake cha onyo la tsunami, iliyotangazwa baada ya tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 8 kwenye vipimo vya Richter kupiga karibu na Visiwa vya Kermadec karibu na pwani ya kaskazini mashariki suiku ya Alhamisi, shirika la kitaifa la Usimamizi wa Majanga (NEMA) limesema leo Ijumaa.
Imechapishwa:
Mawimbi ya tsunami yenye kasi ndugo yameshuhudiwa na shirika la kitaifa la Usimamizi wa Majanga (NEMA) limesema katika jarida lake kwamba "wakaazi wote wanaweza kurudi nyumbani."
Tahadhari ya tsunami pia imeondolewa huko New Caledonia, Waziri wa Ufaransa mwenye dhamana Outre-mer, Sébastien Lecornu ametangaza kwenye Twitter.
Un fort séisme a eu lieu il y a quelques minutes au large de la Nouvelle-Zélande, à 8h28 (heure locale). En lien avec les autorités compétentes et les services de l’État, les alertes tsunami sont déclenchées sur les îles concernées.
— Sébastien Lecornu (@SebLecornu) March 4, 2021
Mapema leo, mamlaka imetoa wito kwa wakaazi kuendelea kuwa waangalifu, na awali shirika la kitaifa la Usimamizi wa Majanga (NEMA) liliwashauri wakaazi wa baadhi ya maeneo ya pwani kuhamia sehemu salama zenye urefu wa juu.