Pata taarifa kuu
UHISPANIA-MARIDHIANO

Kukamatwa kwa Carles Puigdemont: Mchakato wa maridhiano wawekwa hatarini

Tukio la kukamatwa kwa Carles Puigdemont huko Sardinia nchini Italia  Alhamisi tarehe 23 Septemba imezua mtafaruku katika serikali kuu ya Pedro Sánchez. Tukio hili linaweza kuhatarisha mchakato wa mazungumzo ya wazi kati ya Waziri Mkuu wa Uhispania na serikali ya Barcelona.

Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez akizungumza huko New York katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Septemba 23, 2021.
Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez akizungumza huko New York katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, Septemba 23, 2021. AP - Eduardo Munoz
Matangazo ya kibiashara

Hayo yanajiri wakati viongozi wa Italia wameamua kumuachilia Carles Puigdemont na kusema kuwa yuko huru kuondoka nchini humo au kubaki.

Kwa upande wake, chama cha mrengo wa kulia,  kimeghadhabishwa na hatua hiyo ya Italia ya kumuachilia huru  kiongozi huyo wa zamani wa Catalonia.

Habari za kukamatwa kwa Carles Puigdemont huko Sardinia Alhamisi jioni zilimshangaza kiongozi wa serikali kuu Pedro Sánchez. Na hali hii, haifanyi mambo kuwa rahisi kwake, ameripoti mwandishi wetu François Musseau kutoka Madrid.

Pedro Sánchez alianzisha mchakato wa mazungumzo na utawala unaotaka kujitenga wa Barcelona. Lengo ni kuboresha maridhiano na utawala wa Barcelona, kufikia makubaliano juu ya miradi mikubwa ya uwekezaji huko Catalonia, kuboresha aina ya ushuru katika jimbo hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.