Pata taarifa kuu

Rais wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen yuko nchini Ukraine

Rais wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen amewasili mjini Kyiv kujadiliana na rais Volodymr Zelensky  kuhusu mchakato wa nchi yake kujiunga katika Umoja wa Ulaya.

Ziara ya Jumamosi ni ya sita kwa von der Leyen nchini Ukraine tangu vita kati yake na Urusi kuanza
Ziara ya Jumamosi ni ya sita kwa von der Leyen nchini Ukraine tangu vita kati yake na Urusi kuanza © YVES HERMAN / REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Kyiv iliwasilisha maombi ya kupewa uanachama wa EU siku chache tu baada ya uvamizi wa Urusi mnamo Februari 24, 2022.

Kupitia ukurasa wake wa X, zamani ukiitwa Twitter, kiongozi huyo ameongeza kuwa watajadili suala la msaada wa kifedha wa EU kujenga upya Ukraine kama demokrasia ya kisasa na yenye mafanikio.

Ziara ya Jumamosi ni ya sita kwa von der Leyen nchini Ukraine tangu vita kati yake na Urusi kuanza.

Ziara hiyo inakuja huku kukiwa na wasiwasi kwamba uungwaji mkono kwa Ukraine kutoka kwa washirika wake huenda ukapungua kutokana na mapigano yanayoendelea huko Mashariki ya kati.

Von der Leyen ameeleza  kuwa safari yake ilikuwa imepangwa kwa muda mrefu na kwamba ilikuwa ni ziara ya kitamaduni kufanya kabla ya kuwasilisha ripoti kuhusu kupokea wanachama wapya wa EU.

Nchi wanachama wa EU wamekuwa wakiiunga Ukraine mkono katika vita vyake dhidi ya Urusi
Nchi wanachama wa EU wamekuwa wakiiunga Ukraine mkono katika vita vyake dhidi ya Urusi AP - Stefan Rousseau

Waziri wa mambo ya nje wa Ukraine Dmytro Kuleba aliwaambia waandishi wa habari wiki hii kwamba Kyiv iko mbioni kutimiza wajibu wake wa kufungua mazungumzo kuhusu uanachama wa Umoja wa Ulaya, na von der Leyen alikiri mwezi Septemba kwamba Kyiv imepiga hatua kubwa katika jitihada zake za kuwa mwanachama wa EU.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.