Pata taarifa kuu

EU na Uingereza zakubaliana kuhusu biashara na Ireland Kaskazini

NAIROBI – Uingereza na Umoja wa Ulaya, zimeafikiana kuhusu mkataba mpya wa kushirikiana kibiashara na Ireland Kaskazini.

Waziri mkuu wa Uingereza Rish Sunak na Mkuu wa tume ya EU Ursula von der Leyen
Waziri mkuu wa Uingereza Rish Sunak na Mkuu wa tume ya EU Ursula von der Leyen AP - Dan Kitwood
Matangazo ya kibiashara

Hii imekuja baada ya Uingereza kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya maarufu kama Brexit mwaka 2020.

Waziri Mkuu Rishi Sunak, amesifia maafikiano hayo.

“Makubaliano ya leo yanahakikisha kwamba kuna hali nzuri ya kufanya biashara nchini Uingereza, yanalinda masilahi ya Ireland Kaskazini katika muungano wetu.” amesema Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak

Ireland Kaskazini ni sehemu ya Uingereza, lakini inapakana na Ireland ambayo ni mwanachama wa Umoja wa Ulaya, hali ambayo ilikuwa inazua sintofahamu kuhusu ushirikiano wa kibiashara.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.