URUSI- UKRAINE- MAPIGANO
EU kuendelea kuisaidia Ukraine kupambana na Urusi
Rais wa kamisheni ya umoja wa Ulaya, Ursula von de Leyen, ameahidi umoja huo kuendelea kuisaidia Ukraine kwa vifaa vya kisasa vya kijeshi, wakati huu taifa hilo likiendelea kushambuliwa na Urusi.
Imechapishwa:
Cheza - 00:32
Matangazo ya kibiashara
Akihutubia mkutano wa jukwaa la kiuchumi mjini Davos, Uswis, Von de Leyen, amesema kamwe hawatorudia nyuma kuisaidia Ukraine, akionya mwishowe haki itapatikana.
“Kwa karibu mwaka mmoja sasa, Ukraine imeushangaza ulimwengu, wakati huu uvamizi ulipoanza.” amesema Ursula Von De Leyen.
Rais wa Ukraine amekuwa ameendelea kuyataka mataifa ya magharibi kumpa silaha zaidi ilikupigana na uvamizi wa Ukraine nchini mwake.