Pata taarifa kuu
Urusi - Tehran - Diplomasia

Iran : Putin afanya ziara nchini Tehran

Rais wa Urusi,  Vladimir Putin, anafanya ziara nchini Tehran, ikiwa ziara ya pili kwake tangu taifa lake lianze uvamizi nchini Ukraine.


Rais wa Urusi Vladimir Putin akiingia kwenye ukumbi
Rais wa Urusi Vladimir Putin akiingia kwenye ukumbi AP - Kirill Kallinikov
Matangazo ya kibiashara

Putin anatarajiwa kukutana na kiongozi wa Tehran, Ayatollah Ali Khamenei, na rais wa Uturuki  Recep Tayyip Erdogan.

Baadhi ya maswala yanayotarajiwa kujadiliwa na viongozi hao watatu ni pamoja na uzaji wa ngano, hali nchini Ukraine na Syria.

Tangu kuanza kwa vita nchini Ukrain, rais Putin, amekuwa kifanya ziara kwa mataifa yaliokuwa chini ya muungano wa Soviet, mwezi uliopita akizuru mataifa ya Tajikistan naTurkmenistan.

Ziara ya Putin nchini Tehran inatoa nafasi kwake kuimarisha uhusiano kati ya mataifa hayo mawili, ambayo yote yamewekewa vikwazo vya kiuchumi na wenzao wa magharibi.

Ziara hii pia inajiri kipindi hiki, Tehran ikituhumiwa na Marekani kwa kuwa na njama kuipa Urusi ndege za kivita ambazo hazina rubani kutumika kwa vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.