Pata taarifa kuu
UINGEREZA-NATO-USALAMA

Usalama: Viongozi wa NATO wakutana kwa mazungumzo London

Viongozi kutoka nchi zinazounda Umoja wa jeshi la kujihami kwa nchi za Magharibi NATO, wanakutana jijini London kujadili masuala mbalimbali ya usalama na ushirikiano kati yao.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan (kushoto) na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron (kulia) wanatarajia kujelezea kwenye mkutano wa kilele wa NATO (picha ya kumbukumbu).
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan (kushoto) na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron (kulia) wanatarajia kujelezea kwenye mkutano wa kilele wa NATO (picha ya kumbukumbu). LUDOVIC MARIN / POOL / AFP
Matangazo ya kibiashara

Mkutano huu unafanyika nchini Uingereza, siku kumi kabla ya Uchaguzi Mkuu nchini humo.

Tayari Rais wa Marekani Donald Trump amewasili jijini London, na kuelekea katika mkutano huu amekuwa akijigamba kuwa, tangu aingie madarakani, nchi wanachama wa NATO zimeimarisha uwajibikaji wao, kinyume na ilivyokuwa zamani.

Kabla ya kufunguliwa rasmi kwa mkutano huo wa sabini wa NATO, Rais Trump na viongozi wengine wa dunia, watakuwa na dhifa na Malkia wa Uingereza Elizabeth wa pili.

Mbali na mkutano huo wa NATO, viongozi wengine wa dunia kama vile Kansela wa Ujerumani Angela Merkel, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, wanatarajiwa kukutana pembezoni mwa mkutano huo kujadili ushirikiano kati ya nchi zao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.