Pata taarifa kuu
DRCongo-Mauaji

Jeshi la jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo FARDC lafaulu kurejesha hali ya utulifu jijini Kinshasa baada ya kutokea uvamizi uliogharimu maisha ya watu zaidi ya sabini

Serikali ya Jamhuari ya Kidemokrasia ya Congo imesema waasi zaidi ya sabini wamepoteza maisha katika tukio la kuviteka vituo muhimu vya utawala wa rais Joseph Kabila. Kundi la vijana wanaojinasibu kuwa wafuasi wa mwanasiasa Pasta Joseph Mukungubila Mutombo ambaye aliwahi kuwania urais mwaka 2006 nchini humo na  ameiambia RFI kwamba wafuasi wake walikuwa wameandamana nchi nzima kupinga uonevu unatekelezwa na utawala wa Kinshasa.

Vikosi vya FARDC karibu na kituo cha  RTNC,jijini Kinshasa, 30 desemba 2013.
Vikosi vya FARDC karibu na kituo cha RTNC,jijini Kinshasa, 30 desemba 2013. AFP PHOTO/STRINGER
Matangazo ya kibiashara

Serikali ya DRCongo imesema watu sabini wamepoteza maisha wakiwemo wanajeshi watatu katika tukio hilo na jeshi limefaanikiwa kutuliza ghasia hizo zilizo shuhudiwa kwenye maeneo tofauti ya jiji ukiwemo uwanja wa ndege, kituo cha Radio na Runinga ya taifa pamoja na eneo la makao makuu ya jeshi.

Vurugu hizo zilianzia katika mji mkuu Kinshasa ambapo kundi la vijana waliokuwa na silaha za jadi ambao walikiteka kituo cha runinga ya taifa RTNC wakati kikiperusha matangazo yake moja kw amoja huku waandishi wa habari wawili wakashuhudiwa moja kwa moja wakifanyiwa vitisho na vijana hao wa Pasta Joseph Mukungubila ambaye aliwahi kuwania urais mwaka 2006 na kwa sasa anajiita kuwa nabii wa bwana.

Msemaji wa serikali ya DRCongo Lambert Mende amesema jeshi la serikali linadhibiti hali ya mambo, na kwamba uchunguzi umeanzishwa ili kubaini viongozi walionyuma ya vijana hao waasi.

Ghasia kama hizo zimeshuhudiwa pia katika miji ya Kindu na Lubumbashi na kusababisha kukatishwa kwa shughuli za usafiri wa kimataifa kwenye uwanja wa ndege wa Njili. Akizungumza na RFI idhaa ya Kifaransa pasta Joseph Mukungubila Mutombo amesema wafuasi wake hawakuwa na silaha.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.