Pata taarifa kuu

Imetimia miaka mwili tangu Urusi ilipoivamia Ukraine

Nairobi – Tarehe 24 ya mwezi Februari mwaka wa 2022, Urusi ilitekeleza uvamizi nchini Ukraine, ikianzisha vita vikubwa zaidi barani Ulaya tangu vita vya pili vya dunia.

Ukraine imeapa kupata ushindi dhidi ya uvamizi wa Urusi katika ardhi yake wakati huu vita hivyo vikiingia katika mwaka wake wa pili
Ukraine imeapa kupata ushindi dhidi ya uvamizi wa Urusi katika ardhi yake wakati huu vita hivyo vikiingia katika mwaka wake wa pili AP - Efrem Lukatsky
Matangazo ya kibiashara

Miaka miwili baadae, bado hakujaonekana matumaini ya kumalizika kwa mapigano hayo.

Wachambuzi wa masuala ya kimataifa wanasema kuwa mwaka huu wa 2024 utashuhudia makabiliano makali, Ukraine ikitarajia kuchukua maeneo yake yanayokaliwa na Urusi.

Ukraine imeendelea kutoa wito kwa nchi washirika wake kuihami zaidi
Ukraine imeendelea kutoa wito kwa nchi washirika wake kuihami zaidi REUTERS - STRINGER

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kupitia mtandao wake wa X, ameeleza kuwa nchi yake haitachoka kuiiunga mkono Ukraine katika vita vyake na Urusi.

Ukraine imeapa kupata ushindi dhidi ya uvamizi wa Urusi katika ardhi yake wakati huu vita hivyo vikiingia katika mwaka wake wa pili.

Hatua ya Kyiv kujilinda dhidi ya mashambulio ya Moscow imeonekana kulemazwa na ukosefu wa usambazaji wa silaha inazohitaji kutoka kwa washirika wake nchi za Magharibi.

Wakuu wa nchi za G7 wanatarajiwa kukutana kwa njia ya mtandaoni kuadhimisha miaka miwili ya vita hivyo, rais Volodymyr Zelensky akiwa miongoni mwa watakaohudhuria.

Waziri mkuu wa Italia Giorgia Meloni ni miongoni wa washirika wa Kyiv ambao wamewasili nchini Ukraine kwa maadhimisho ya miaka mwili ya vita, akitarajiwa kuongoza kikao cha mtandaono cha wakuu wa G7.

Giorgia Meloni, Waziri Mkuu wa Italia amewasili nchini Ukraine
Giorgia Meloni, Waziri Mkuu wa Italia amewasili nchini Ukraine via REUTERS - UKRAINIAN RAILWAYS

Tayari nchi ya Uingereza imetangaza msaada wa Euro milioni 245 kwa nchi ya Ukraine kuisaidia kupata silaha inazohitaji kwa dharura.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.