Pata taarifa kuu
UFARANSA-UKRAINE-URUSI

Macron asema Urusi haipaswi kushinda vita dhidi ya Ukraine

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameisthumu Urusi kwa kujaribu kukwamisha utaratibu wa Kimataifa kwa kukwamisha kusambaa kwa chakula duniani, na kusema kuwa nchi hiyo haipaswi kushinda vita vinavyoendelea.

Rais wa Ufaransa  Emmanuel Macron akizungumza kwenye mkutano wa G 7 nchini Ujerumani, Juni 28 2022
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akizungumza kwenye mkutano wa G 7 nchini Ujerumani, Juni 28 2022 AP - Markus Schreiber
Matangazo ya kibiashara

“Urusi haipaswi kushinda vita hivi, na vikwazo vitasalia kwa muda mrefu,” amesema.

Akizungumza wakati wa kuufunga mkutano wa G 7 nchini Ujerumani, ambako viongozi wa nchi hizo wameahidi kutoa Dola Bilioni 5 kusaidia kusuluhisha uhaba na kupanda bei ya chakula duniani.

“Ufaransa nayo itatoa msaada wa Euro 700,000 kuhakikisha kuna usalama wa chakula,” ameongeza.

Usalama umeimarishwa kwenye mkutano huo ambao kwa kisiasa kikubwa utazungumzia vita vya Ukraine na Urusi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.