Wahamiaji: "Hali ya Dharura" katika nchi za Balkan
Umoja wa Ulaya umeitisha kikao cha dharura na viongozi wa nchi za Ulaya zinazokabiliwa na wimbi la wahamiaji na wakimbizi, kwa mfano wa nchi ndogo ya Slovenia, ambayo imekua ikijaribu kuandaa, kwa shida, sehemu ya kupitia katika ardhi yake.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Marais na viongozi wa Serikali za Austria, Bulgaria, Croatia, Ujerumani, Ugiriki, Hungary, Romania, Makedonia, Serbia na Slovenia watakutana Jumapili jijini Brussels kwa kujaribu kuratibu hatua yao kwa kukabiliana na "hali ya dharura" katika nci za Balkan , Tume ya Ulaya imesema.
Umoja wa Ulaya umetolewa wito na Ljubljana kusaidia ikiwa ni pamoja na kuweka uzio dhidi ya wahamiaji nchini Hungary Slovenia, Serbia na Croatia, moja ya nchi kuu wanakopitia wahamiaji na wakimbizi wakielekea kaskazini mwa Ulaya.
Rais wa Tume ya Ulaya, Jean-Claude Juncker ameelewa matatizo makubwa (...) ambayo karibu yote yapo, ambapo moja ya nchi hizo "inakabiliana nayo", Slovenia yenye wakazi milioni mbili ilijikuta inawapokea wahamiaji 21,500 tangu Jumamosi juma lilopita.
Jumatano wiki hii, takriban wahamiaji 11,000 miongoni mwao wamepokelewa katika makambi yalioandaliwa kwa ajili ya shughuli hiyo kwa kusubiri waendelea na safari yao hadi Austria, mpaka wa kaskazini wa Slovenia.