Pata taarifa kuu
HUNGARY-AUSTRIA-WAKIMBIZI-USALAMA

Maelfu ya wahamiaji waelekea Austria kwa mguu

Maelfu ya wahamiaji wameondoka mapema leo Ijumaa alasiri kutoka kituo kikuu cha treni cha Budapest wakijaribu kutembea kwa mguu wakielekea "Austria", baada ya viongozi wa Hungary kuchukua uamzi Jumanne wiki hii wa kusimamisha usafiri wa kimataifa kwa kutumia reli, ameshuhudia mwandishi wa AFP.

Maelfu ya wahamiaji waondoka kwa mguu kutoka kituo kikuu cha treni cha Budapest wakielekea kwenye mpaka wa Austria, Septemba 4, 2015.
Maelfu ya wahamiaji waondoka kwa mguu kutoka kituo kikuu cha treni cha Budapest wakielekea kwenye mpaka wa Austria, Septemba 4, 2015. AFP/AFP
Matangazo ya kibiashara

Wahamiaji, ambao baadhi yao walikuwa wamekwama katika mji mkuu wa Hungary kwa siku kadhaa, wamesema wanataka kutembea kwa mguu hadi kwenye mpaka wa Austria, ulio kwenye umbali wa kilomita 175, wakati serikali ya Budapest imeongeza jitihada za kuwahamisha kinyume na matakwa yao katika makambi ya mapokezi ya kwanza.

Wahamiaji, ikiwa ni pamoja na watoto na watu wanaotumia viti vya magurudumu, wamevuka moja ya daraja kuu katika mji wa Danube bila hofu ya kukamatwa na vikosi vya usalama.

Hungary, moja ya nchi kuu wanakopitia wahamiaji kwa kwenda Ulaya ya Kati, kuulionekana wahamiaji wapya 3,300 wakiwasili kwa siku moja pekee ya Alhamisi, shirika la Umoja wa Mataifa linalowahudumia wakimbizi limebaini leo Ijumaa.

Wakati huo huo Aylan, mtoto mdogo kutoka syria aliyefariki baada ya kuzama katika bahari wakati alipokua akijaribu kukimbia kufuatia mapigano nchini Syria, amezikwa le Ijumaa na familia yake, lakini tukio hilo la kusikitisha ambalo ni ishara kwa mgogoro wa wahamiaji limeendelea kuzua migawanyiko kati ya nchi za Ulaya.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.