Waisrael 4 wajeruhiwa katika shambulizi la kisu kusini mwa Israel
Waisrael 4 wamejeruhiwa katika shambulio la kisu lililotekelezwa leo Jumamosi katika mji wa Kiryat Gat kusini mwa Israeli, polisi ya Israel imetangaza.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Waisrael hao 4 ni Wayahudi, na mmoja wao alijeruhiwa vibaya, vyanzo vya matibabu vimebaini.Miongoni mwa watatu, mmoja anasumbuliwa na majeraha madogo tu.
Polisi imelitaja shambulizi hilo kuwa ni la "kigaidi", na kuongeza kuwa imeanza kumsaka msambuliaji ambaye alitimka baada ya kitendo hicho, na kwa sasa hajulikani aliko.
Mashambulizi ya visu yamekithiri katika Ukanda huo hususan katika Ukingo wa Magharibi, na katika mji wa Jerusalem (Mashariki).
Mashambulizi haya ya visu, makabilano kati ya vijana wa Palestina na askari wa Israel na vurugu kati ya wakazi wa Palestina na walowezi wa Israel yamewaua Wapalestina 86, ikiwa ni pamoja na Muisrael mwenye asili ya Kiarabu na Waisrael 15 pamoja na Mmarekani mmoja na raia mmoja wa Eritrea , kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na shirika la habari la Ufaransa la AFP.