Matangazo ya BBC na VOA yapigwa marufuku Burundi
Serikali ya Burundi imeonya na kuchukua hatua ya kupiga marufuku matangazo ya mashirika ya utangazaji ya BBC na VOA kwa muda wa miezi sita kuanzia Mei 7 mwaka huu.
Imechapishwa:
Mashirika haya ya utangazaji yanashtumiwa na serikali ya Burundi kutofuata sheria zinazotoa muongozo wa uandishi habari nchini.
Serikali ya Burundi naishutumu BBC kwa kushindwa kumwajibisha mwanaharakati wa Burundi katika mahojiano aliyofanyiwa katika idhaa ya kifaransa ya shirika hilo.
Mtandao wa habari unaoegemea upande wa serikali ya Burundi, Ikiriho, kwenye ukurasa wake wa Twitter, umerusha nyaraka ya taarifa hiyo.
URGENT ???? Les radios @BBC et @VOANews sont suspendues de diffusion au #Burundi pendant 6 mois à partir du 7 mai 2018 "pour manquement à la loi régissant la presse".
Ikiriho (@Ikiriho) May 4, 2018
La rubrique "Annonces" du @LeRenouveauBdi suspendue pour 3 mois pour diffusion dans une langue non-déclarée au CNC pic.twitter.com/aZkk34wCka
Radio kadhaa za kibinfasi zimeharibiwa na kufungwa nchni humo wakati wa mzozo wa kisiasa ulioanza mnamo 2015, wakati rais Nkurunziza aliposhinda muhula wa tatu madrakani, uliozusha mgogoro wa kisiasa na kusababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na wengine kuyahama makazi yao. Watu zaidi ya 3000 wamezuiliwa katika jela mbalimbali kwa mujibu wa mashirika ya kiraia nchini humo.