Mvua yasababisha mafuriko makubwa jijini Nairobi, uharibifu waripotiwa
Nchini Kenya, jiji kuu la Nairobi linashuhudia mafuriko makubwa kutokana na mvua inayoendelea kunyesha, kama ilivyo kwenye nchi jirani za Afrika Mashariki.
Imechapishwa:
Barabara zimejaa maji, huku baadhi ya mitaa iliyo Mashariki mwa jiji hilo, ikifurika na kusababisha wakaazi kushindwa kuingia wala kuondoka.
Serikali inasema tangu mvua kubwa ilipoanza kunyesha mwezi Aprili, watu zaidia ya 30 wamepoteza maisha nchini humo, likiwemo jiji kuu Nairobi.
Mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa nchini humo, imekuwa ikitoa tahadhari ya kushuhudia kwa mvua kubwa, na sasa inasema mbali na mafuriko, huenda kukashuhudiwa maporomoko ya ardhi.
“Mvua itaendelea kunyesha sana. Tuna mashaka kuwa huenda kukatokea na maporomoko ya ardhi,” amesema, David Gikungu, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo.
Following other rescue operations in Mathare, Githurai 45 and other places in Nairobi, we have also rescued 96 people at Graceland in Athi River following yesterday night's heavy downpour.
— Kenya Red Cross (@KenyaRedCross) April 24, 2024
This was made possible through the collaborative efforts of a multi-agency rescue team… pic.twitter.com/Z5cmz4elwa
Serikali inasema imechukua tahadhari kuwasaidia raia wa nchi hiyo, waliothiriwa.
“Maafisa wetu wa uokoaji wapo katika maeneo yaliyoathiriwa kuwasaida, watu walioathirika,” amesema naibu msemaji wa serikali Gabriel Mutuma.
GABRIEL MUTHUMA MINI MODULE 24 04 2024
Pius Masai mtalaam wa kukabiliana na majanga nchini Kenya, anasema serikali ndio ya kulaumiwa baada ya mafuriko kujaa mitaani.
“Maafisa wa serikali walikuwa wapi, wakati wananchi walipokuwa wanajenga kwenye mkondo wa maji ?,” amehoji katika mazungumzo yake na RFI Kiswahili.
MODULE PIUS MASAI KUHUSU MAFURIKO
Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha pia zimetatiza shughuli za kawaida katika miji mingine ya Afrika Mashariki kama Dar es salaam nchini Tanzania, ambako barabara zimejaa maji, sawa na Bujumbura huku tahadhiri ikitolewa kwa wakaazi kuchukua tahadhri na kuhamia maeneo yaliyoinuka.