Pata taarifa kuu

Serikali ya Kenya yatakiwa kufanya juhudi za kudhibiti maambukizi zaidi ya UKIMWI

Dunia , Inapoadhimisha siku ya kimataifa kuhusu mapambano ya UKIMWI, mashirika ya kiraia yanayopambana na Ukimwi nchini Kenya yanahofu hatua zilizopigwa  miaka 20, kudhibiti mambukizi mapya na vifo vinavyotokana na Ukimwi, huenda zikahujumiwa katika kipindi hiki cha janga la Corona.

Nchini Kenya, wanawake makahaba huchangia karibu 15% kwa maambukizi mapya ya UKIMWI.
Nchini Kenya, wanawake makahaba huchangia karibu 15% kwa maambukizi mapya ya UKIMWI. Georgina Goodwin / AFP
Matangazo ya kibiashara

Tangu kuripotiwa kisa cha Kwanza cha virusi vya HIV nchini Kenya ,miaka 37 iliyopita, hatua muhimu zimepigwa kupambana na janga la UKIMWI na kudhibiti madhara yake.

Hata hivyo masharika ya kiraia nchini Kenya yanahisi hatua hizo chanya zinatishiwa na mvutano kati ya serikali na wafadhili

Patricia Asero ambaye ameishi na virusi vya HIV kwa zaidi ya  miaka 20 anahofu kuwa  hali iliyoshuhudiwa katika miaka ya nyuma, si kitu angependa kijurudie.

Vidonge vya Dolutegravir vinavyotumika kutibu wagonjwa wa UKIMWI nchini Kenya, Juni 2017.
Vidonge vya Dolutegravir vinavyotumika kutibu wagonjwa wa UKIMWI nchini Kenya, Juni 2017. REUTERS/Baz Ratner

Na  wanaharakati wanaopambana na Ugonjwa wa Kifua kikuu (TB) mojawapo  ya magonjwa tegemezi miongoni mwa watu  wanaoishi na virusi vya HIV nao wanaisihi serikali kutoipa nafasi TB kusababisha vifo zaidi .

Baraza linaloongoza mapambano dhidi ya UKIMWI Kenya, limerpoti maambukizi mapya  zaidi ya elfu 41 mwaka wa 2021, huku kasi ya maambukizi ikiwa ni asilimia 4.9 . Idadi ya watu wanaoishi na virusi vya HIV nchini Kenya ni zaidi ya milioni moja nukta tatu

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.