Uganda
Bobi Wine akamatwa na polisi Kampala
Mwanasiasa wa upinzani na aliyekuwa mgombea urais Robert Kyagulanyi, anayefahamika kwa jina maarufu Bobi Wine, amekamatwa jijini Kampala akiongoza maandamano kushinikiza kupatikana kwa wafuasi wake, waliotoweka.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Watu kadhaa wamekamatwa wakiwemo wabunge zaidi ya kumi kutoka chama cha Bobi Wine cha National Unity Platformkulingana na duru kutoka kambi ya upinzani.
Vikosi vya usalama vilifyatua mabomu ya kutoa machozi na kutawanya waandamaji waliokuwa wameandamana na mwanasiasa huyo.
Bobi Wine anadai kuwa wafuasi wake walikamatwa na wakati wa kipindi cha kuelekea na baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Januari.