Pata taarifa kuu

Pelosi aitaka China kutokuwa na wasiwasi wowote kuhusiana na ziara yake Taiwan

Spika wa bunge la  Marekani Nancy Pelosi, amekutana na rais wa Taiwan, Tsai Ing-wen  ambapo kabla ya hapo, allihotubia bunge na kusisitiza  kuwa ziara yake ni ya kuimarisha urafiki kati ya nchi hizo mbili. 

Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani Nancy Pelosi akiwa na Rais wa Taiwan Tsai Ing-wen tarehe 3 Agosti 2022 mjini Taipei, mji mkuu wa Taiwan.
Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani Nancy Pelosi akiwa na Rais wa Taiwan Tsai Ing-wen tarehe 3 Agosti 2022 mjini Taipei, mji mkuu wa Taiwan. © Taiwan Presidential Office via AP
Matangazo ya kibiashara

Pelosi ameipongeza Taiwan kwa kuwa nchi  huru duniani na kwamba anajisikia vizuri kuitwa  rafiki wa Taiwan. 

Aidha, amesema , ziara yake inalenga kutafuta namna ya nchi yake inavyoweza  kuimarisha usalama na Taiwan ,kuinua uchumi na kuboresha ushirikiano wa mabunge yote mawili.  

Baada ya hotuba hiyo ,spika Pelosi amekutana  na rais Tsai Ing- Wen ambaye amempa zawadi ya medali maalum  ya kutambua juhudi zake kuongeza mawasiliano  kati ya Washington na Taipei. 

Ziara ya Pelosi imekosolewa na  China ,iliyokuwa imetoa onyo kali kwa Taiwan iwapo itampokea kiongozi huyo wa juu wa Marekani. China inaendelea kusisitiza, Taiwan ni sehemu ya nchi yake na sio huru. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.