Washington na Berlin wakasirikia Serbia kwa kununua silaha kutoka China
Umoja wa Ulaya na Marekani zimekasirishwa na kitendo cha China kuipa silaha za kudungua ndege Serbia. Silaha hizo zilitolewa na kusafirishwa mwishoni mwa juma na ndege za kijeshi za China.
Imechapishwa:
Wikendi hii, ndege kubwa ya kijeshi ya China ilitua katika uwanja wa ndege wa Belgrade, Serbia, na kusababisha mtafaruku, kwa kuwa ilikuwa ni usafirishaji wa silaha nchini kutoka China. Ndege hiyo huenda ilikuwa na makombora ya FK3, ambayo ununuzi wake ulijadiliwa mwaka wa 2019.
Hatua ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani inaonekana kama tishio. "Serbia ni nchi huru, lakini lazima ifahamu athari na hatari katika muda mfupi na mrefu," Washington ilisema siku ya Jumanne.
Kutofautiana na sera ya ulinzi ya Umoja wa Ulaya
Serbia, ambayo inataka kujiunga na Umoja wa Ulaya, ni nchi ya kwanza barani humo kuitaka China kujitayarisha na mifumo hii ya hali ya juu na mkanganyiko huo pia umebainishwa na Ujerumani. Berlin inasema inasubiri kuona wanataka mpango huo kuoanisha sera yao ya ulinzi na ile ya Umoja wa Ulaya, EU.
Kwa miaka kadhaa, Serbia imeonyesha uhusiano wake na Urusi na China. Belgrade tayari iko chini ya shinikizo kutokana na msimamo wake usioeleweka kuhusu vikwazo dhidi ya Urusi.
Kwa hivyo Serbia inaombwa kutoonyesha uhusiano wake na Beijing, wakati uhusiano kati ya China na nchi za Magharibi unaweza kuwa mbaya katika mazingira ya vita vya Ukraine.