Pata taarifa kuu
BURUNDI-MAJANGA ASILI

Maporomoko yaua watu wengi Kaskazini Magharibi mwa Burundi

Watu zaidi ya 20 wameripotiwa kufariki dunia kutokana na maporomoko ya mlima yaliyoangukia makazi ya watu katika kijiji cha Nyabundu, tarafani Mugina mkoani Cibitoke Kaskazini Magharibi mwa Burundi.

Nchi nyingi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na Kenya na Burundi, zimeendelea kukumbwa na mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Hapa ni katika eneo moja la Kenya mwaka 2007.
Nchi nyingi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na Kenya na Burundi, zimeendelea kukumbwa na mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Hapa ni katika eneo moja la Kenya mwaka 2007. AFP/Brenda Bannon
Matangazo ya kibiashara

Kulingana na vyombo vya habari nchini Burundi, mpaka sasa idadi ya watu waliofariki kufuatia maporomoko hayo haijajulikana bado.

Redio Isanganiro imeripoti kuwa watu 24 wamefariki dunia kufuatia maporomoko hayo.

Lakini msemaji wa Wizara ya Usalama Pierre Nkurikiye, amesema hajapata ipoti rasmi ya vilivyoharibiwa na maporomoko hayo yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha nchini humo.

Taarifa kutoka eneo la Nyabundu zinasema mvua nyingi zilizonyesha usiku wa Jumatano kuamkia Alhamisi zilisababisha maporomoko ya ardhi na kumomonyoka kwa mlima mmoja ulio katika eneo hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.