Jordan: Mwana Mfalme Hamzah ahusishwa katika jaribio la mapinduzi
Jordan imesema imefakiwa kuzuia jaribio la mapinduzi dhidi ya uongozi wa Kifalme lililomhusisha kaka wa Mfalme Abdulah wa pili.
Imechapishwa:
Watu 16 wamekamatwa kufuatia jaribio hilo na wanadaiwa kushirikiana na watu wa kigeni kujaribu kumwondoa madarakani Mfalme Abdullah.
Mshukiwa Mkuu ni aliyekuwa Mwana Mflame Hamzah bin Hussein aliyeondolewa katika nafasi hiyo mwaka 2004. Anadaiwa kutishia usalama wa Kifalme.
Hata hivyo Malkia Nour wa Jordan ambaye ni mama wa mrithi wa zamani wa ufalme, Mwana Mfalme Hamzah al-Hussein, amesema madai yanayomkabili mwanawe kwamba alihusika katika vitendo vya kutatiza usalama nchini humo, ni fitina ya kumuharibia jina tu. Nour, ambaye ni mama wa kambu wa mfalme wa sasa wa Jordan, Abdullah wa Pili, alisema katika ujumbe aliouandika katika mtandao wa Twitter, kwamba anaomba "ukweli na haki ujitokeze kwa wale wote waliochafuliwa jina."
Mwanafalme Faisal bin Farhan Al Saud ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia, ameimbia France 24 kuwa Saudi Arabia inaunga mkono hatua zilizochukuliwa na mshirika wake Jordan.