Pata taarifa kuu
MAREKANI-AFGHANISTAN-SIASA-USALAMA

Washington yaipunguzia misaada Afghanistan kutokana na mvutano wa kisiasa

Marekani imetangaza kwamba itapunguza dola bilioni 1 kwa msaada iliyokuwa ikiitolea Afghanistan, na iko tayari kufanya vivyo hivyo mnamo mwaka 2021 baada ya rais wa Afghanistan Ashraf Ghani na mpinzani wake Abdullah Abdullah kushindwa kuunda serikali mpya.

Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo baada ya mkutano wao na waandishi wa habari kwenye Ikulu ya rais huko Kabul, Julai 9, 2018.
Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo baada ya mkutano wao na waandishi wa habari kwenye Ikulu ya rais huko Kabul, Julai 9, 2018. Andrew Harnik/Pool via Reuters
Matangazo ya kibiashara

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Mike Pompeo amethibitisha taarifa hiyo na kubaini kwamba Marekani ilikuwa na matumani kwamba Afghanistan sasa inaelekea pazuri

Ashraf Ghani na Abdullah Abdullah wote walidai kuwa walishinda uchaguzi uchaguzi wa urais uliofanyika Septemba 28, ambao uligubikwa na tuhuma za udanganyifu, matatizo ya kiufundi na vurugu.

"Pia tutaanza kutathmini programu zetu na miradi yetu yote ili kupunguza zaidi misaada yetu kwa Afghanistan na tutafikiria tena ahadi zetu kwa minajili ya mikutano ya wafadhili ijayo kwa Afghanistan," imesema taarifa ya Pompeo iliyotolewa baada ya mazungumzo yaliyofanyika huko Kabul.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.