URUSI-SYRIA-AJALI
Ndege ya Urusi yaanguka Syria na kusababisha vifo vya abiria 32
Ndege ya Urusi imeanguka katika uwanja wa ndege wa kijeshi katika mkoa wa Latakia nchini Syria na kusababisha vifo vya abiria wote 32.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wizara ya Ulinzi imethibitisha kutokea kwa ajali hiyo siku ya Jumanne.
Ndege hiyo ilikuwa na abiria 26 na wahudumu 6 akiwemo rubani.
Inaelezwa kuwa sababu ya ajali hii inaaminiwa kuwa ni hitilafu ya kimitambo.
Aidha, Urusi inasema ndege hiyo haikushambuliwa.