Pata taarifa kuu
UTURUKI-SYRIA-USALAMA

Zaidi ya watu 300 wakamatwa nchini Uturuki

Uturuki imetangaza leo Jumatatu kwamba imewakamatwa watu zaidi ya 300 ambao wamekosoa kwenye mitandao ya kijamii jeshi la nchi hiyo kuzindua mashmabulizi kaskazini magharibi mwa Syria.

Polisi ya Uturuki imeendesha msako unaowalenga watu waliokosoa jeshi kuzindua mashambulizi nchini Syria.
Polisi ya Uturuki imeendesha msako unaowalenga watu waliokosoa jeshi kuzindua mashambulizi nchini Syria. Reuters
Matangazo ya kibiashara

Tangu kuzuka kwa operesheni iliyoitwa "Mazao ya Zabibu" dhidi ya wanamgambo wa Kikurdi katika eneo la Afrin, mamlaka ya Uturuki imeonya kwamba itawashughulikia wanaopinga, wanaokosoa au kupotosha utaratibu wa jeshi kuingilia kati.

Katika taarifa iliyotolewa leo Jumatatu, wizara ya mambo ya ndani imesema kuwa watu 311 walifungwa siku hizi 10 zilizopita kwa"kueneza propaganda ya kigaidi".

Uturuki inawachukulia wanamgambo wa Kikurdi YPG kama kundi la kigaidi na vuguvugu la chama cha PKK, ambalo lilichukua silaha nchini Uturuki mnamo mwaka 1984.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.