Pata taarifa kuu
KENYA-ELIMU-MOTO

Serikali nchini Kenya yasema bweni la wanafunzi liliteketezwa makusudi

Waziri wa Elimu nchini Kenya Fred Matiang'i amesema moto uliozuka katika bweni la Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya Moi jijini Nairobi, na kusababisha vifo vya wanafunzi tisa na wengine kujeruhiwa ulianzishwa kwa makusudi.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya  Moi jijini Nairobi
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya Moi jijini Nairobi thestar
Matangazo ya kibiashara

Matiang'i ameeleza kuwa uchunguzi wa awali umeonesha wazi kuwa, mkasa huo haukuwa ajali na tayari polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi.

Aidha, Waziri huyo ambaye pia anakaimu kama Waziri wa Usalama, ameeleza kuwa Polisi wamemfahamisha kuwa wamepata taarifa za uhakika kuonesha kuwa moto huo ulianzishwa makusudi.

Shule hiyo imefungwa kwa wiki mbili, wakati huu wanafunzi, wazazi na walimu wakiendelea kuomboleza.

Mwaka uliopata, mabweni ya shule za sekondari 100 yaliteketezwa moto katika visa ambavyo pia viliripotiwa kuwa vya makusudi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.