Rais Magufuli azindua daraja mpya Kigamboni-Dar
Rais wa Tanzania John Magufuli amezindua daraja mpya la Kigamboni jijini Dar es salaam lenya urefu wa Kilimota 680 inayounganisha eneo la Kurasini na Kigamboni.
Imechapishwa:
Daraja hilo ambalo limepewa jina la Nyerere, mwanzilishi wa taifa hilo liligharimu Dola za Marekani 128 kwa msaada wa serikali ya China.
Akizundua daraja hilo, rais Magufuli ameeleza kuwa watumiaji wa daraja hilo hasa wale walio na pikipiki, baskeli na magari watalipia lakini wale wanaotumia miguu watapita bure.
Katika hatua nyingine, rais Magufuli amewaambia Watanzania kuwa ataendelea kuwachukulia hatua wafanyikazi wa serikali ambao hawawajibiki iapsavyo kazini.
Amewataka watumishi wa Umma wasioweza kuendana na kasi yake waondoke.