Pata taarifa kuu

Kenya: Odinga asema hatozungumza na Ruto bila mpatanishi

Nchini Kenya, kiongozi wa upinzani Raila Odinga amesema hatazungumza na rais William Ruto bila ya kuwepo kwa mpatanishi kwa kile anaeleza kuwa kiongozi huyo haaminiki.

Kinara wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga wakati wa mkesha wa kuwakumbuka wafuasi wake wao waliouawa wakati wa maandamano
Kinara wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga wakati wa mkesha wa kuwakumbuka wafuasi wake wao waliouawa wakati wa maandamano AFP - SIMON MAINA
Matangazo ya kibiashara

Msimamo huu wa Odinga unakuja baada ya Ruto kusema kuwa, yupo tayari kukutana na kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na mpinzani wake baada ya kushuhudiwa maandamano ya wiki kadhaa, kupinga kupanda kwa gharama ya maisha, miongoni mwa mambo mengine, yaliyosababisha maafa na majeruhi ya waandamanaji.

Upinzani ulifanya mkesha kuwakumbuka wafuasi wake waliouawa katika maandamano
Upinzani ulifanya mkesha kuwakumbuka wafuasi wake waliouawa katika maandamano REUTERS - MONICAH MWANGI

Odinga alisitisha maandamano yaliyokuwa yafanyike nchi nzima na kuwataka wafuasi wake kutumia wiki hii kuwaomboleza watu waliopoteza maisha wakati huu akipanga kulishtaki jeshi la polisi kwenye Mahakama ya Kimataifa ya ICC kwa kuwaua waandamanaji.

Lakini je? Kuna utashi wa kisiasa katika hili? Dokta Bryan wanyama ni mtaalamu wa siasa za Kenya na mhadhiri katika chuo kikuu cha kibabii kilichopo Bungoma.

‘‘Cha msingi hapa Kenya ni yetu sisi sote na wakati kama huu ni muhimu wakati ndugu wawili wanapokuwa na matatizo wakae pamoja kutafuta suluhu.” alisma Dokta Bryan wanyama.

00:36

Dokta Bryan wanyama ni mtaalamu wa siasa

Muungano wa upinzani unalaumu ukatili wa polisi kwa vifo hivyo, lakini wizara ya mambo ya ndani imetetea hatua iliyochukuliwa na maofisa wa usalama kuwakabili waandamanaji.

Mapema siku hiyo, viongozi wa upinzani, akiwemo Odinga, walizuru hospitali mbalimbali jijini Nairobi kuwatembelea watu waliojeruhiwa wakati wa maandamano hayo.

Mwanasiasa wa upinzani Kalonzo Musyoka alisema ni muhimu haki ipatikane kwa ajili yao.Tangazo kuhusu maandamano zaidi litatolewa Ijumaa, alisema.

Upinzani unasema utahakikisha waliojeruhiwa na kuawaua wakati wa maandamano wanapata haki
Upinzani unasema utahakikisha waliojeruhiwa na kuawaua wakati wa maandamano wanapata haki © Azimio la Umoja

Wanadiplomasia na makundi ya kutetea haki za binadamu wameitaka serikali na upinzani kutatua tofauti zao kwa amani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.