Pata taarifa kuu
SYRIA

Watu 70 wauwawa nchini Syria siku chache kabla ya ziara ya Kofi Annan nchini humo

Zaidi ya watu 70 wameuwawa nchini Syria jana Ijumaa,wakati makumi ya maelfu ya waandamanaji wakiandamana mitaani huku mizinga ikitumika kuwatawanya waandamanaji katika mji wa Damascus, waangalizi nchini humo wamesema.

Mjumbe wa Umoja wa mataifa na jumuiya ya nchi za kiarabu katika mgogoro wa Syria Kofi Annan.
Mjumbe wa Umoja wa mataifa na jumuiya ya nchi za kiarabu katika mgogoro wa Syria Kofi Annan. REUTERS/Tiksa Negeri
Matangazo ya kibiashara

Machafuko hayo mapya yametokea wakati mjumbe wa umoja wa mataifa na jumuiya ya nchi za Kiarabu Kofi Annan ambaye anaongoza mpango wa kusitisha mapigano nchini humo akikamilisha mpango wa kurejea Damascus.

Wanadiplomasia mjini Geneva wamesema kuwa katibu mkuu huyo wa zamani wa Umoja wa mataifa anataraji kuzuru mji mkuu wa Syria mapema wiki ijayo.

Kofi Annan amekuwa akiongoza mpango wa kumaliza machafuko na umwagaji damu nchini Syria, mpango ambao hata hivyo umekuwa ukivunjwa mara kadhaa.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.