Venezuela yafunga mpaka wake na Brazil
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameamuru kufungwa kwa mpaka wa kusini mwa nchi yake, ambao unaitenganisha na Brazil. Hatua hii imeanza kutumika usiku wa kuamkia leo (saa za Venezuela).
Imechapishwa:
Uamuzi huu umechukuliwa kutokana na kile rais wa Venezuela amekiita "uchokozi" kutoka serikali ya mrengo wakulia ya Brazil.
Venezuela pia inafuatilia kwa karibu hali kwenye mpaka wake na Colombia, rais wa Venezuela ameongeza.
"Sitaki kuchukuwa aina hiyo ya maamuzi, lakini ninajifunza uwezekano wa kuchukuwa hatua kama hiyo, kufunga mpaka wa Venezuela na Colombia," amesema Maduro.
Colombia na Brazil wamejiunga na upinzani wa mrengo wa kulia nchini Venezuela kwa msimamo wao mmoja wa kumtimuwa rais Maduro na chama ccha Kisoshalisti cha PSUV.