Pata taarifa kuu
VENEZUELA-MAREKANI-URUSI-SIASA

Marekani na Urusi zawasilisha azimio kuhusu Venezuela

Marekani na Urusi zimewasilisha maazimio yanayokinzana kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya kisiasa nchini Venezuela.

Wajumbe wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa wakipiga kura.
Wajumbe wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa wakipiga kura. UN Photo/Loey Felipe
Matangazo ya kibiashara

Marekani inamtaka rais Nicolas Maduro kukubali kufayika kwa Uchaguzi mpya wa urais haraka iwezekanavyo, lakini pia kuhusu misaada ya kibinadamu kuingia nchini humo.

Hata hivyo, Marekani haijasema inataka uchaguzi huo ufanyike lini, wakati huu ikiitaka jumuiya ya Kimataifa kumuunga mkono kiongozi wa upinzani Juan Guido kama kiongozi wa Venezuela.

Hata hivyo, Urusi nayo inataka katika azimio lake, mataifa ya nje yaache kuingilia siasa za ndani ya Venezuela na rais Nicolas Maduro, atambuliwe kuwa rais halali wa nchi hiyo.

Kwa namna ya mambo yalivyo, Marekani na Urusi zinatarajiwa kutumia kura zao za veto, kuzuia maazimio hayo.

Katika hatu nyingine, kiongozi wa upinzani ameonya dhidi ya serikali ya rais Maduro kukataa kuruhusu misaada ya kibinadamu kuingia nchini humo, wakati uo huo Maduro akionya kuwachukua hatua kali wale watakaojaribu kuleta vurugu katika nchi yake.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.