Pata taarifa kuu
SUDANIKUSINI-SIASA-USALAMA

Mvutano waibuka kuhusu uundwaji wa serikali Sudani Kusini

Chama cha South Sudan National Democratic Movement nchini Sudan Kusini, kimeunga mkono wito wa kiongozi wa upinzani Riek Machier, kuahirishwa kwa uundwaji wa serikali ya mpito kwa miezi kadhaa.

Salva Kiir na Riek Machar lSeptemba 12, 2018.
Salva Kiir na Riek Machar lSeptemba 12, 2018. YONAS TADESSE / AFP
Matangazo ya kibiashara

NDM kinasema bado kuna changamoto ya kijeshi na suala la mipaka, mambo ambayo hajapewa ufumbuzi.

Machar ambaye anaishi jijini Khartoum na anayetarajiwa kuwa Makamu wa kwanza wa rais amesema hatorejea Juba, kufanikisha uundwaji wa serikali hiyo mwezi Mei, kwa sababu za kiusalama.

Hata hivyo, rais Kiir amesisitiza kuwa uudwaji wa serikali hiyo utaendelea kama ilivyopangwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.