Ceta: Bunge la Ulaya lapitisha mkataba wa biashara huru na Canada
Bunge la Ulaya limeunga mkono mkataba utakaowezesha nchi za Muungano huo kufanya biashara bila malipo na nchi ya Canada. Mkataba huo umepingwa na wanaharakati wa mazingira, wale kutoka mashirika ya wanunuzi.
Imechapishwa:
Mkataba huu utaanza kutekeelzwa mwezi ujao, suala ambalo limepingwa na wanaharakati ambao wameendamana kuupinga kwa madai kuwa utazua mashindano ya kibiashara nje ya bara la Ulaya.
Rais wa Marekani Donald Trump anaye amepinga mkataba huo.
Baada ya miaka saba ya mjadala na utata, wabunge 408 wamepiga kura katika neema ya hati yenye kurasa 2,000, wabunge 254 walipiga kura dhidi ya hati hiyo na 33 hawakupiga kura, mwandishi wetu katika Brussels, Anastasia Becchio amearifu.
Kama ilivyotarajiwa, wabunge kutoka vyama vya mrengo wa kulia, ikiwa ni pamoja Conservatives, Liberals walipiga kura katika neema ya mkataba huo jumla wa kiuchumi na kibiashara. Wabunge kutoka vyama vya Social Democratic waligawanyika: Wengi wao walipiga kura katika neema ya mkataba huo, lakini wale kutoka Ufaransa, Ubelgiji , Uholanzi na Poland walipiga kura dhidi ya mkataba huo.
Hata hivyo mkataba huo umepingwa na wanaharakati wa mazingira, wale kutoka mashirika ya wanunuzi na vyama vyenye msimamo mkali kutoka mrengo wa kulia na kushoto.