Pata taarifa kuu
ZIMBABWE-MAANDAMANO

Maandamano ya upinzani yatawanywa Zimbabwe

Polisi ya Zimbabwe imetumia mabomu ya machozi na mizinga ya maji kwa kuwatawanya waandamanaji dhidi ya serikali.

waandamanaji dihi ya serikali waandelea na maandamano yao wakipinga kile walichokiita sera za kiuchumi za Rais Robert Mugabe.
waandamanaji dihi ya serikali waandelea na maandamano yao wakipinga kile walichokiita sera za kiuchumi za Rais Robert Mugabe. REUTERS/Philimon Bulawayo
Matangazo ya kibiashara

Karibu waandamanaji 200 wameshutumu kile walichokiita ukatili wa polisi na kutoa wito kwa Rais Robert Mugabe kujiuzulu.

Vyama vya upinzani nchini Zimbabwe vimepanga kufanya maandamano ya pamoja Ijumaa wiki hii mjini Harare.

Maandamano dhidi ya serikali yameongezeka dhidi ya sera za kiuchumi za Rais Robert Mugabe.

Zimbabwe imeachana na sarafu yake ya kitaifa baada ya kukumbwa na mfumuko wa bei kwa asilimia bilioni mwaka 2009.

Mugabe anaongoza Zimbabwe kimabavu tangu nchi hiyo kupata uhuru wake mwaka 1980.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.