Wimbi la Siasa
Ziara ya rais Tshisekedi wa DRC huko CHINA,pia mchakato wa uchaguzi wa 2023
Imechapishwa:
Cheza - 09:59
Makala ya wimbi la siasa wiki hii imeangazia ziara ya rais wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Félix Tshisekedi nchini China, na pia maendeleo ya mchakato wa uchaguzi kwenye nchi hiyo.Waalikwa wetu katika kuzungumzia hili ni Kashando Mukanisa Yvon mchambuzi huru na mtaalamu wa siasa za DRC, wakili Moise Bashwira wa chama cha UNC moja ya vyama madarakani vya Sacred Union, na pia Muhindo Safari Akayezu wa chama cha upinzani cha Ensemble pour la République chake Moise Katumbi. Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kupata mengi zaidi