Pata taarifa kuu

Kenya: Odinga akanusha ripoti kuwa atamuunga mkono Kalonzo 2027

Nairobi – Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, amekunusha ripoti za vyombo vya habari kwamba atamuunga mkono makomo wa rais wa zamani, Kalonzo Musyoka kuwania urais kwenye Uchaguzi wa mwaka 2027.

Kupitia msemaji wake Raila Odinga, amesema sifa alizompa  mwandani wake kisiasa siku ya jumapili hazimaanishi  atamuunga mkono kwenye uchaguzi wa mwaka 2027
Kupitia msemaji wake Raila Odinga, amesema sifa alizompa  mwandani wake kisiasa siku ya jumapili hazimaanishi  atamuunga mkono kwenye uchaguzi wa mwaka 2027 AFP - SIMON MAINA
Matangazo ya kibiashara

Kupitia msemaji wake Raila Odinga, amesema sifa alizompa  mwandani wake kisiasa siku ya jumapili hazimaanishi  atamuunga mkono kwenye uchaguzi wa mwaka 2027 kama ilivyokuwa imerpotiwa na baadhi vya vyombo vya habari.

Odinga amesema ni mapema sana  kutangaza mgombea urais miaka minne kabla ya kufanyika kwa uchaguzi akisema watatangaza mgombea wao mwaka mmoja au miezi kadhaa kabla ya uchaguzi.

Musyoka, ambaye amewahi kuwa Makamu wa rais mara tatu, aliacha azma yake ya kuwania urais na kumuunga mkono Odinga, mara mbili akiwa mgombea mwenza wake
Musyoka, ambaye amewahi kuwa Makamu wa rais mara tatu, aliacha azma yake ya kuwania urais na kumuunga mkono Odinga, mara mbili akiwa mgombea mwenza wake © skmusyoka

Hatua ya Odinga kumumiminia sifa Kalonzo ilitafusiriwa na wengi kwamba huenda mwanasiasa huyo ambaye amewania urais mara kadhaa, atamuunga mkono Kalonzo kwenye uchaguzi ujao, ila pia imebainika kuwa vyama tanzu vya muungano wa upinzani havifurahishwa na kauli ya Odinga kuonesha wazi huenda akamuunga mkono Kalonzo kwenye uchaguzi ujao, hatua inayotishia kusambaratisha upinzani.

Musyoka, ambaye amewahi kuwa Makamu wa rais mara tatu, aliacha azma yake ya kuwania urais na kumuunga mkono Odinga, mara mbili akiwa mgombea mwenza wake.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.