Pata taarifa kuu

Kenya: Upinzani wamuonya balozi wa Marekani kuhusu uchaguzi uliopita

Nairobi – Viongozi wa muungano wa upinzani nchini Kenya, Azimio, wamemjia juu balozi wa Marekani nchini humo, Meg Whitman, ambaye wakati wa kongamano la ugatuzi alidai uchaguzi uliopita ulikuwa huru na haki akikosoa uchochezi wa vurugu.

Katika hotuba yake wakati wa mkutano kuhusu ugatuzi nchini Kenya, Odinga amemuonya balozi wa Marekani nchini humo kwa kuingilia masuala ya ndani ya taifa
Katika hotuba yake wakati wa mkutano kuhusu ugatuzi nchini Kenya, Odinga amemuonya balozi wa Marekani nchini humo kwa kuingilia masuala ya ndani ya taifa © Raila Odinga
Matangazo ya kibiashara

Kiongozi wa upinzani Raila Odinga wakati akihutubia kongamano hilo mjini Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu katika mkoa wa bonde la ufa siku ya Alhamisi, alimkashifu Whitman kwa kile alichodai kuwa anaingilia masuala ya Kenya.

Mkuu huyo wa upinzani alimwambia mjumbe huyo wa Marekani alipokuwa akitetea maandamano ya hivi majuzi ambayo alisema yalitimiza madhumuni ya kuunganisha nchi na kulazimisha serikali kuja kwenye meza ya mazungumzo.

Balozi wa Marekani amekashifiwa na upinzani kwa matamshi yake kuwa uchaguzi nchini Kenya ulikuwa huru na wa haki
Balozi wa Marekani amekashifiwa na upinzani kwa matamshi yake kuwa uchaguzi nchini Kenya ulikuwa huru na wa haki © Raila Odinga

Kinara wa muungano huo, Raila Odinga, sasa anamtaka balozi Meg kukaa kimya ama vinginevyo watashinikiza arudishwe nchini mwake.

“Waache Wakenya walivyo, kama maandamano yanaweza kusababibisha mazungumzo kati ya Ichung`wah na Kalonzo basi maandamano ni mazuri, Kenya sio Marekani au mkoloni mwa Marekani, funga mdomo wako ukiwa hapa hali si hivyo tutashinikiza urejeshwe kwenu.” alisema Odinga.

00:20

Raila Odinga kuhusu balozi wa Marekani

Aidha Odinga alisisitiza kuwa iwapo Whitman ataendelea kutoa maoni yake kuhusu masuala ya Kenya, basi huenda mrengo wa kisiasa wa upinzani ukalazimika kuiomba serikali ya Marekani kumuondoa kwenye taifa hilo.

Magavana na washika dau kuhusu ugatuzi nchini Kenya wanakutana katika mkoa wa bonde la ufa kujadili hatua ambazo zimepigwa tangu serikali za majimbo kuaanza
Magavana na washika dau kuhusu ugatuzi nchini Kenya wanakutana katika mkoa wa bonde la ufa kujadili hatua ambazo zimepigwa tangu serikali za majimbo kuaanza © Raila Odinga

Matamshi yake Odinga yanajiri baada ya yale ya wabunge wa upinzani ambao walimkashifu balozi huyo, huku baadhi yao wakimsihi abatilishe maoni yake ambayo walisema yalikuwa kinyume na uungaji mkono wa Marekani kwa demokrasia.

Wabunge hao pia walidai kuwa matamshi ya Whitman yanaweza kudhoofisha mazungumzo ya kitaifa yanayoendelea kati ya serikali na upinzani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.