Pata taarifa kuu

Serikali ya Kenya na upinzani kuaanza mazungumzo

Nairobi – Serikali ya Kenya na upinzani hivi leo wanatarajiwa kuanza mazungumzo yanayolenga kutafuta muafaka baada ya maandamano ya vurugu kupinga uchaguzi uliopita pamoja na kupanda kwa gharama ya maisha.

Raila Odinga kiongozi wa upinzani nchini Kenya, pamoja na rais  William Ruto
Raila Odinga kiongozi wa upinzani nchini Kenya, pamoja na rais William Ruto © AFP
Matangazo ya kibiashara

Mazungumzo haya yanayoenda kuratibiwa na rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, yanatarajiwa kutoa suluhu ya mvutano unaoendelea kati ya kinara wa upinzani Raila Odinga na Serikali, ambapo kila upande ulichagua timu ya watu watano.

Rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo ndiye mratibu wa mazungumzo hayo
Rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo ndiye mratibu wa mazungumzo hayo © dailypost

Muungano wa upinzani Azimio uliongoza maandamano mwezi Machi na Julai dhidi ya utawala wa rais William Ruto kupinga kile walichosema ni kupanda kwa gharama ya maisha na kutaka mageuzi katika tume ya uchaguzi kwenye taifa hilo la Afrika Mashariki.

Maandamano hayo yalionekana kuzidi baada ya serikali kutangaza kuongezwa kwa ushuru katika baadhi ya bidhaa kwa kile rais Ruto alisema hatua hiyo inalenga kuimarisha maendeleo nchini mwake.

Polisi walikabiliana na wafuasi wa upinzani wakati wa maandamano yaliofanyika jijini Nairobi kupinga kupanda kwa gharama ya maisha awali
Polisi walikabiliana na wafuasi wa upinzani wakati wa maandamano yaliofanyika jijini Nairobi kupinga kupanda kwa gharama ya maisha awali REUTERS - JOHN MUCHUCHA

Makundi ya kutetea haki za binadamu nchini humo yanasema karibia watu 30 walifariki katika maandamano hayo wakati upinzani ukisema rekodi zake zilionyesha watu 50 waliuawa.

Timu ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga inataka kujadili gharama ya maisha na mageuzi ya uchaguzi baada ya kushindwa katika uchaguzi mwaka jana, lakini serikali inasisitiza kuwa tayari inafanya kazi kurekebisha mfumuko wa bei na kupunguza gharama ya bidhaa za kimsingi.

Upinzani ulisimamisha maandamano mwezi Aprili na Mei ili kuruhusu mchakato sawa wa mazungumzo ya pande mbili, lakini maandamano yalianza tena baada ya mazungumzo kuvunjika.

Upinzani unaituhumu serikali kwa kupanda kwa  bei za bidhaa
Upinzani unaituhumu serikali kwa kupanda kwa bei za bidhaa AFP - YASUYOSHI CHIBA

Ruto na Odinga wamesema hawatafanya mazungumzo  yoyote ya kugawana mamlaka.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.