Pata taarifa kuu

Upinzani nchini Kenya wasema umekubaliana na serikali kuzungumza

Muungano wa upinzani nchini Kenya, Azimio la Umoja, umesema umekubaliana na serikali, kuunda kamati ya watu 10 ili kujadili na kutatua changamoto zinazoikabili nchi hiyo.

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga AFP - SIMON MAINA
Matangazo ya kibiashara

Taarifa hiyo imetolewa Jumamosi  jioni hii na kiongozi wa muungano wa upinzani bungeni, Opiyo Wandayi, ambaye amefafanua kuwa, maafikiano hayo yamekuja baada ya kushauriana na wenzao wa muungano wa Kenya Kwanza.

Aidha, Wandayi ameeleza , mazungumzo hayo yataongozwa na kusimamiwa  na rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo, na yanalenga kutatua changamoto kati ya serikali na upinzani kwa manufaa ya wananchi wa Kenya.

Kila upande utatoa watu watano, kuunda kamati hiyo. Taarifa hiyo pia imethibitishwa na upande wa serikali, kupitia kiongozi wake bungeni, Kimani Ichung'wah.

Hata hivyo, haijafahamiki ni lini mazungumzo hayo yataanza.

Kauli hii ya upinzani inakuja baada ya wiki kadhaa za maandamano kupinga sheria ya fedha, iliyosababisha kupanda kwa gharama ya maisha. Maandamano hayo yalisababisha vifo vya watu zaidi ya 30 na mamia kujeruhiwa kwa mujibu wa mashirika ya Kimataifa ya kutetea haki za binadamu nchini humo.

Wiki hii  Odinga alidokeza kuwa, rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alijaribu kumpatanisha na Ruto bila mafanikio huku rais William Ruto akisema yuko tayari kwa mazungumzo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.