Pata taarifa kuu

Wakenya wanamatumaini ya kumalizika kwa maandamano ya upinzani

Nairobi – Raia wa Kenya wameelezea matumaini yao ya kumalizika kwa mzozo wa kisiasa ambao umelikumba taifa hilo la Afrika Mashariki baada ya rais kusema kwamba yuko tayari kufanya kikao na kiongozi wa upinzani Raila Odinga wakati “wowote.

Rais wa Kenya William Ruto ameonyesha nia ya kuwa tayari kwa mazungumzo na kinara wa upinzani Raila Odinga
Rais wa Kenya William Ruto ameonyesha nia ya kuwa tayari kwa mazungumzo na kinara wa upinzani Raila Odinga AFP - LUIS TATO
Matangazo ya kibiashara

Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga, aliitisha maandamano mwezi Machi ambapo hadi sasa mrengo wake umeshirki maandamano kwa siku tisa dhidi ya utawala wa rais Ruto.

Maandamano hayo yamegubikwa na machafuko pamoja na makabiliano makali baina ya wafuasi wa upinzani na maofisa wa polisi nchini humo.

Kupitia ukurasa wake wa twitter rais Ruto, ameonyesha nia yake ya kufanya mazungumzo na Odinga.

Hadi tukichapisha taarifa hii, Odinga ambaye amewataka Wakenya kujitokeza kwa mkesha siku ya Jumatano kwa ajili ya kuwakumbuka waandamanaji waliouawa kwenye maandamano hayo, hajazungumzia wito wa mkuu wa nchi.

Vurugu hizo zimezua hasira miongoni mwa makundi ya kutetea haki za binadamu, polisi wakituhumiwa  kwa kurusha mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe.

Amnesty inasema raia wameuawa na wengine kujeruhiwa wakati wa maandamano
Amnesty inasema raia wameuawa na wengine kujeruhiwa wakati wa maandamano AP - Brian Inganga

Watu 20 wameuawa, kulingana na takwimu rasmi, ingawa Azimio (upinzani) unasema angalau watu 50 wamekufa.

Baadhi ya raia nchini humo haswa wafanyibiashara wanasema maandamano hayo yanatatiza biashara zao wakati baadhi ya wafuasi wa upinzani wakiwa na mtazamo tofauti.

Maeneo mbalimbali yalisitisha biashara wakati wa maandamano ya upinzani
Maeneo mbalimbali yalisitisha biashara wakati wa maandamano ya upinzani REUTERS - THOMAS MUKOYA

Odinga, ambaye anadai uchaguzi wa urais wa mwaka jana ulikarabatiwa ameilaumu serikali kwa kupanda kwa gharama ya maisha ambapo pia amewatuhumu maofisa wa polisi na serikali kwa ukatili dhidi ya waandamanaji.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.