Pata taarifa kuu

Kenya : Niko tayari kwa mazungumzo na upinzani : Rais Ruto

Nairobi – Rais wa Kenya William Ruto amesema, yupo tayari kukutana na kuzungumza na kiongozi wa upinzani Raila Odinga, wakati wowote baada ya wiki kadhaa za maandamano dhidi ya serikali yake, na kusababisha maafa na majeruhi yanayoripotiwa kutekelezwa na polisi.

Mrengo wa Odinga umekuwa ukiaanda maandamano kwa kile unachosema ni kupanda kwa gharama ya maisha
Mrengo wa Odinga umekuwa ukiaanda maandamano kwa kile unachosema ni kupanda kwa gharama ya maisha AFP - SIMON MAINA
Matangazo ya kibiashara

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Ruto amemwambia Odinga kuwa, yupo tayari kukutana na Odinga.

Hatua hii ya Ruto imekuja baada ya Odinga hapo jana kusema kuwa, kulikuwa na jitihada za kumpatanisha na Ruto chini ya rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan wiki mbili zilizopita, lakini juhudi hizo ziligonga mwamba.

‘‘Kumekuwa na jitihada kutoka nje kuona iwapo kuna uwezekano wa kufanyika kwa mazungumzo na sasa naweza kusema wazi hapa kwamba rais wa Tanzania alikuwa hapa wiki mbili zilizopita baada ya kualikwa na rais Ruto kujaribu kutusaidia katika mazungumzo lakini akasubirishwa na upande wa rais Ruto kwa siku mbili.’’

00:54

Kinara wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga

Odinga anasema hatua hiyo ya serikali ilichangia kuondoka kwa rais wa Tanzania nchini humo bila ya kukutana na viongozi hao.

Upinzani ambao umekuwa ukiitisha maandamano kulalamikia kupanda kwa gharama ya maisha nchini humo, umesitisha maandamano yaliyokuwa yafanyike leo kote nchini na badala yake imesema siku hii itatumiwa kuwaomboleza watu waliouawa mikononi mwa polisi.

Tayari shirika la kutetea haki za binadamu nchini humo, KNCHR, ambalo lilibuniwa na bunge, limesema linasikitisha kushuhudia ukiukaji wa haki za binadamu kutoka kwa waandamanaji waharibifu na polisi.

Polisi walikabiliana na wafuasi wa upinzani wakati wa maandamano yaliofanyika jijini Nairobi kupinga kupanda kwa gharama ya maisha awali
Polisi walikabiliana na wafuasi wa upinzani wakati wa maandamano yaliofanyika jijini Nairobi kupinga kupanda kwa gharama ya maisha awali REUTERS - JOHN MUCHUCHA

Wiki iliyopita, shirika la Amnesty International, lilishtumu kile lilitaja kuwa ukandamizaji kutoka kwa polisi na kusema walikuwa na ushahidi wa mauaji ya watu 27 katika mwezi Julai pekee.

Wakosoaji wanamtuhumu Ruto kuenda kinyume cha ahadi alizozitoa wakati kampeni za uchaguzi wa Agosti mwaka uliopita, alipoahidi kuimarisha uchumi na maisha ya wakenya kupitia mfumo wa kuwainua raia wa chini maarufu kama Bottom up.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.