Pata taarifa kuu

Kenya: Maombi ya kuwakumbuka waliofariki  katika maandamano yamefanyika

Nairobi – Nchini Kenya, wakaazi katika baadhi ya maeneo yakiwemo Kisii, Magharibi ya Kenya, Nairobi na Mombasa pwani ya taifa hilo la Afrika Mashariki , leo Jumatano wamewasha mishumaa na kufanya maombi kwa ukumbusho wa Wakenya waliofaririki wakati wa maandamani ya upinzani kulaani kupanda kwa gharama ya maisha.

Ibada za ukumbusho wa wafuasi wa upinzani waliouawa katika maandamano imefanyika katika maeneo tofauti nchini Kenya
Ibada za ukumbusho wa wafuasi wa upinzani waliouawa katika maandamano imefanyika katika maeneo tofauti nchini Kenya © Gladys Wanga
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii inakuja baada ya upinzani nchini humo kutangaza kusitisha maandamano yaliokuwa yamepangwa kufanyiak juma hili.

“Tumekuja kuwasha mishumaa kuwakumbuka watu waliofariki baada ya kupigwa risasi na polisi wakati wa maandamano dhidi ya serikali. Pia tungependa kuwakumbusha polisi kwamba hatuna shida nao bali tunatekeleza haki yetu ya kikatiba pekee,” mmoja wa  wakaazi wa Kisii, Magharibi ya Kenya amesema.

Katika taarifa iliyotolewa na Muungano wa Azimio (Upinzani) Julai 25, wananchi katika maeneo mbalimbali nchini humo wametakiwa kuwasha mishumaa na kuweka maua katika maeneo mbalimbali ya makutano yakiwemo ya mbuga, hospitali, vituo vya mabasi na makanisa ili kuonyesha upendo na heshima yao kwa wahanga wa maandamano dhidi ya serikali.

Katika taarifa nyingine ya Julai 24, upinzani ulisema kwamba "nchi kwa sasa inakabiliwa na hali isiyokuwa ya kawaida ya ukatili wa polisi, na Serikali inawatumia watu wenye silaha ili kuzima maandamano."

Upinzani ulitangaza kusitisha maandamano kuwakumbuka wafuasi wake waliouawa wakati wa maandamano
Upinzani ulitangaza kusitisha maandamano kuwakumbuka wafuasi wake waliouawa wakati wa maandamano © Gladys Wanga- Gavana Homabay

Tume ya kitaifa ya haki za binadamu katika taifa hilo pia ililaani vitendo vya ukatili wa polisi vilivyosababisha watu kupoteza maisha wakati wa maandamano, madai ambayo wizara ya usalama wa ndani inaendelea kukanusha.

Mnamo Jumanne, Julai 25, katibu mkuu katika wizara ya mambo ya ndani na kitaifa Raymond Omollo alitangaza kwamba afisa  sheria mmoja wa polisi aliuawa na wengine 305 kujeruhiwa wakati wa maandamano ya Azimio.

Kwa upande mwengine viongozi wa upinzani wakiongozwa na Raila Odinga, wametembelea baadhi ya wafuasi wao waliojeruhiwa ambao wamelazwa katika hosipitali tofauti jijini Nairobi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.