Kambi ya Ruto wana imani ya kupata haki mahakamani
Nchini Kenya, wakati huu aliyekuwa mgombea urais kupitia muungano wa kisiasa wa Azimio la Umoja One Kenya, Raila Odinga akitarajiwa kufika kwenye Mahakama ya Juu kupinga ushindi wa mpinzani wake, William Ruto, aliyekuwa mgombea mwenza wake, Martha Karua amesema, wana imani watapata haki Mahakamani, lakini pia wataheshimu uamuzi wa Mahakama.
Imechapishwa:
Chama cha Jubilee kimewaonya viongozi waliochaguliwa kupitia chama hicho kuwa wapo hatarini kupoteza nyadhifa zao iwapo watajiunga na muungano wa kisiasa wa Kenya Kwanza, unaoongozwa na rais mteule William Ruto.
Onyo hili limekuja baada ya baadhi ya viongozi waliochaguliwa kupitia chama cha UDM kutoka muungano wa Azimio la Umoja One Kenya wake mwanasiasa mkongwe Raila Odinga, kuhamia upande wa Ruto siku ya Alhamisi.