Pata taarifa kuu
TANZANIA-HAKI

Kiongozi wa chama cha CHADEMA Freeman Mbowe afikishwa mahakamani

Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania, Freeman Mbowe, amefikishwa kwenye Mahakama Kuu kufunguliwa mashtaka ya ugaidi, ambayo chama chake cha upinzani CHADEMA kinasema yamechochewa kisiasa.

Kiongozi wa chama cha CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake wakizungumza na Mawakili wao katika Mahakama Kuu Division ya Uhujumu Uchumi Leo Agosti31, 2021.
Kiongozi wa chama cha CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake wakizungumza na Mawakili wao katika Mahakama Kuu Division ya Uhujumu Uchumi Leo Agosti31, 2021. © CHADEMA Tanzania/Twitter.com
Matangazo ya kibiashara

Tangu Julai 21, Mbowe mwenye umri wa miaka 59 amekuwa akizuiwa baada ya kukamatwa jijini Mwanza akijiandaa kuwahotubia wanachama wa chama chake kushinikiza mabadiliko ya Katiba.

Wakati huo huo mawakili wa Freeman Mbowe wameiomba mahakama kumuachilia huru mteja wao wakidai mahakama hiyo haina mamalaka kisheria kusikiza kesi hiyo.

Peter kibatala anayeongoza jopo la mawakili wa Mbowe amewaambia waandishi habari kuwa endapo hoja zao zitakataliwa, wataendelea kuwapigania wateja wao kutumia vifungu vya sheria.

Shauri hilo lililosikilizwa kwa zaidi ya saa tatu limehudhuriwa na viongozi wengine wa vyama vya upinzani na wawakilishi wa baadhi ya balozi ikiwemo Uingereza na Marekani, asasi za kiraia na viongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.