Marekani
Rais Obama apinga mkataba wa bomba la mafuta.
Rais wa Marekai Barrack Obama, amekataa kutia saini mradi kati ya Marekani na Canada wa kujenga bomba la mafuta kutoka Canada humo hadi Texas.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Rais Obama amesema pandekezo hilo limetupiliwa mbali baada ya kukosa muda wa kutosha wa kuutathimini kwa ndani zaidi na wananchi kuhusishwa kikamilifu.
Wapinzani wa rais Obama kutoka chama cha Republican ambao wamekuwa wakipinga mradi huo,walikuwa wamempa makataa ya siku 60 kuamua hatima ya mradi huo ambao ungegharimu serikali ya Obama Dola Bilioni 7.