USHIRIKIANO-DIPLOMASIA
Urusi: Vladimir Putin akubali mwaliko wa Kim Jong-un kuzuru Korea Kaskazini
Rais wa Urusi Vladimir Putin amekubali kwenda Korea Kaskazini kwa mwaliko wa kiongozi wake Kim Jong-un, ambaye kwa sasa anazuru hasa nchini Urusi kuimarisha uhusiano wao wa kijeshi. Kwa sasa, hata hivyo, hakuna chochote ambacho kimewasilishwa rasmi kuhusiana na uwezekano wa makubaliano ya kutoa vifaa vya kijeshi kwa Urusi ili kusaidia mashambulizi yake nchini Ukraine, kama ilivyotajwa na Washington.
Imechapishwa: