Pata taarifa kuu
ULINZI-DIPLOMASIA

Kwa nini India ndio muagizaji mkuu wa silaha duniani

Siku ya Alhamisi, Machi 16, New Delhi iliweka agizo la vifaa vya kijeshi kwa kiasi cha euro bilioni 8. Makombora, helikopta, mizinga na mifumo ya ulinzi ya kielektroniki… huu ni mkakati wa kijeshi wa India.

Mfumo wa makombora wa Akash wa Jeshi la India ulionyeshwa wakati wa mazoezi ya kusherehekea Siku ya Jamhuri mnamo Januari 23, 2023 huko New Delhi.
Mfumo wa makombora wa Akash wa Jeshi la India ulionyeshwa wakati wa mazoezi ya kusherehekea Siku ya Jamhuri mnamo Januari 23, 2023 huko New Delhi. AFP - MONEY SHARMA
Matangazo ya kibiashara

Kutoka kwa mwanahabari wetu mjini Bangalore,

Mnamo Jumatatu Machi 13, Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Amani ya Stockholm (SIPRI) ilichapisha ripoti yake ya kila mwaka kuhusu silaha. Wakati India iliweka agizo kubwa la zana za kijeshi wiki hii, kulingana na  ripoti ya SIPRI, nchi hiyo ndiyo nchi inayoingiza silaha nyingi zaidi duniani.

India inakabiliwa na masharti mawili yanayokinzana. Kwa upande mmoja, kuongeza uwezo wake wa kijeshi kwa haraka dhidi ya tishio kutoka China kwenye mipaka yake na katika eneo la Indo-Pasifiki na dhidi ya Pakistan. Kwa upande mwingine, inafanikiwa kutengeneza silaha kwenye ardhi yake badala ya kuziagiza kutoka nje, ndani ya mfumo wa mpango mkuu wa "India inayojitosheleza" iliyotangazwa na Waziri Mkuu, Narendra Modi. Lakini ni wazi kwamba "Make in India" haina kweli kusimamia maendeleo katika uwanja wa kijeshi.

Siemon Wezeman wa Taasisi ya Stockholm, anaeleza hivi: “Tangu mwisho wa Vita Baridi, India imekuwa nchi inayoongoza ulimwenguni kuagiza silaha. Haiwezi kukabiliana na matatizo ya kiufundi ya uzalishaji kwenye ardhi yake. Sekta ya silaha ya serikali ni ya polepole na ya urasimu. Kombora la BrahMos, lililoagizwa hivi karibuni, kwa mfano limetengenezwa nchini Urusi. "

Katika kipindi cha 2018-22, India ilichangia 11% ya uagizaji wa silaha zote duniani, mbele ya Saudi Arabia (9.6%).

Urusi, tangu enzi za Umoja wa Kisovieti, imekuwa mshirika muhimu sana na muuzaji wa kijeshi kwa New Delhi. Vita nchini Ukraine havina madhara yoyote kwa India kwa usambazaji wake wa silaha na nafasi yake ya kijiografia na kisiasa: India imekuwa ikikabiliwa na ucheleweshaji wa uwasilishaji tangu Urusi ilipojihusisha na vita; lakini kwa upande mwingine, pia inataka kuchukua fursa ya hali mpya ya kisiasa ya kijiografia kuanzisha uhusiano mpya wa kibiashara na Moscow.

Mahusiano mapya ya biashara kwa mafuta ya bei nafuu bila shaka, lakini hiyo inakwenda mbali zaidi. Waziri wa Mambo ya Nje Subrahmanyam Jaishankar ameihakikishia Urusi kwamba ataruhusu kukwepa viikwazo na kulipa kwa fedha za India.

Siemon Wezeman anaamini kwamba mabadiliko makubwa yatachukua muda. "Ni mapema mno kujua kama vita vitapunguza utegemezi wa India kwa Urusi. 

Kulingana na ripoti ya Sipri, Urusi inachangia 45% ya ununuzi wa vifaa vya kijeshi wa India, ikifuatiwa na Ufaransa kwa 29% na Marekani kwa 11%. Badala ya takwimu imara ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.