KOREA KUSINI-KOREA KASKAZINI-USHIRIKIANO
Moon azungumzia njia ya kupata amani katika ukanda wa Korea
Rais wa Korea Kusini Moon Jae-In amesema, eneo la Korea kutokuwa na mradi wa kutengeneza silaha za nyuklia ndio njia pekee ya kupata amani.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Aidha, amesema atakuwa tayari kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un iwapo mazingira yataruhusu ili kuendelea kujadili suala hili.
Kauli ya rais Moon imekuja baada ya mataiafa hayo mawili jirani kuanza mazungumzo siku ya Jumanne kwa mara ya kwanza baada ya mwaka 2015.
Lengo la mazungumzo hayo, ni kwa Korea Kusini kuiruhusu Korea Kaskazini kutuma kikosi cha wanamichezo wake kushiriki mashindano ya olimpiki ya msimu wa baridi mwezi ujao.