Pata taarifa kuu
KOREA KASKAZINI

Korea Kaskazini yataka usawa wa kijeshi na Marekani

Korea Kaskazini jana Jumamosi imesema kuwahaitashushwa chini kwa lolote bali inataka usawa wa kijeshi na hasimu wake Marekani kwa ukamilifu wa silaha za nyuklia, hatua ambayo imelazimisha baraza la Usalama la umoja wa Mataifa kuwa na mazungumzo mapya kuhusu mgogoro huo

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un akishuhudia uzinduzi wa  kombora Hwasong-12 September 16, 2017
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un akishuhudia uzinduzi wa kombora Hwasong-12 September 16, 2017 路透社。
Matangazo ya kibiashara

Kim Jong-Un alifanikiwa siku ya Ijumaa alifanikiwa kurusha kombora la Hwasong-12 la masafa ya kati juu ya Japan, akijibu vikwazo vya karibuni vya Umoja wa Mataifa kuhusu jaribio lake la sita la nyuklia.

 

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litakuwa na mkutano siku ya Alhamisi mkutano ambao utajikita kutafuta namna nzuri ya kutekeleza vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini ili kuondoa kitisho cha kuenea kwa silaha za maanagamizi duniani.

Marekani imeitisha kikao hicho ambacho kitafanyika wakati wa mkutano Mkuu wa kila mwaka wa viongozi wa dunia kwenye Umoja wa Mataifa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.