Pata taarifa kuu
USALAMA-DIPLOMASIA

Machafuko nchini Haiti: Ufaransa kupeleka ndege maalum kuondoa raia wake walio hatarini Haiti

Wakati katika mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince kwa mara nyingine kuliripotiwa majibizano makali ya risasi siku ya Jumamosi Machi 23 na hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbaya siku baada ya siku, Quai d'Orsay imetangaza hivi punde siku ya Jumapili usiku kuanzishwa kwa safari maalum za ndege ili kuwezesha Wafaransa "walio hatarini zaidi" kuondoka nchini Haiti. Safari hizo za ndege zilizokodishwa na Wizara ya Majeshi, zilitarajiwa kuanza siku ya Jumapili.

Maafisa wa Kitengo cha Usalama Mkuu wa Ikulu ya Kitaifa, USGPN, wakitenga eneo la ulinzi karibu na moja ya vituo vitatu vya polisi katikati mwa jiji baada ya polisi kuzima shambulio la genge siku moja kabla huko Port-au-Prince. Prince, huko Haiti, Machi 9, 2024.
Maafisa wa Kitengo cha Usalama Mkuu wa Ikulu ya Kitaifa, USGPN, wakitenga eneo la ulinzi karibu na moja ya vituo vitatu vya polisi katikati mwa jiji baada ya polisi kuzima shambulio la genge siku moja kabla huko Port-au-Prince. Prince, huko Haiti, Machi 9, 2024. AP - Odelyn Joseph
Matangazo ya kibiashara

Kutokana na matukio ya machafuko nchini Haiti, Paris itatoa suluhisho kwa raia wake. Magenge ya uhalifu yanaendelea kusababisha machafuko katika mji mkuu Port-au-Prince.

Uwezo wa kijeshi

Kulingana na habari zetu, operesheni bado hazijaanza. Kwa kusema kweli, huku sio kuhamishwa kwa raia, lakini njia iliyopendekezwa raia kuondoka nchini Haiti wakati usafiri wa anga kwa ndege za kibiashara na Port-au-Prince ukisitishwa. Kwa jumla, Wafaransa 1,100, ikiwa ni pamoja na idadi kubwa ya raia wenye uraia pacha, wanaishi Haiti, kulingana na takwimu za Wizara ya Mambo ya Nje.

Ili kufanya hivyo, helikopta ya kijeshi inapaswa kuwachukua watu wahusika katika eneo ambapo wametakiwa kukusanyika katika mji mkuu wa Haiti kabla ya kuwapeleka kwa kutumia helikopta kubwa kuelekea Martinique au Guadeloupe. Raia "wanaalikwa kuripoti kwa ubalozi wa Ufaransa huko Port-au-Prince kwa nambari +509 29 99 90 90 ikiwa bado hawajafanya hivyo", inabainisha wizara ambayo haikuwa na makadirio ya idadi ya watu husika siku ya Jumapili. Ubalozi wa Ufaransa huko Port-au-Prince bado upo wazi na "unaendelea na shughuli zake licha ya hali kuzorota", inabainisha Wizara ya Mambo ya Nje.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.