Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken kuzuru Paris wiki ijayo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken atazuru Paris wiki ijayo kukutana na viongozi wa Ufaransa, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imsema. Antony Blinken atakutana na wenzake wa Ufaransa "ili kuendelea na majadiliano juu ya kuimarisha uhusiano kati ya Marekani na Ufaransa" baada ya mgogoro wa nyambizi.
Imechapishwa:
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken atazuru Paris wiki ijayo kukutana na viongozi wa Ufaransa, Wizara ya mambo ya Nje imesema Ijumaa (Oktoba 1) baada ya mzozo wa kidiplomasia uliosababishwa na Australia kuvunja mkataba mkubwa wa nyambizi za Ufaransa.
Atakuwa Paris kuanzia Jumatatu hadi Jumatano wiki ijayo kwa mkutano wa Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo (OECD) na "atakutana pia na wenzake wa Ufaransa ili kuendelea na majadiliano juu ya kuimarisha uhusiano muhimu kati ya Marekani na Ufaransa juu ya msururu wa maswala, "ikiwa ni pamoja na" usalama katika eneo la Indo-Pacific, "amesema msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Marekani Ned Price.